Pages

KWA MAWASILIANO ZAIDI- Email ranyikwa@yahoo.com au +255 713 257 793.

Wednesday, October 24, 2012

Waziri Mulugo aiaibisha serikali

• Asema Tanzania ni Muungano wa Zimbabwe, Pemba na Tanganyika
 
na George Maziku



NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, amemwaibisha Rais Jakaya Kikwete na taifa kwa ujumla mbele ya jamii ya kimataifa, baada ya kuitangazia dunia kuwa Tanzania imetokana na muungano wa visiwa vya Zimbabwe na Pemba vilivyoungana na Tanganyika.
Mbali na hilo, aliwaambia mamia ya wajumbe kutoka mataifa mbalimbali katika Bara la Afrika kuwa, Tanzania ilizaliwa mwaka 11964.
"Wasilisho langu litakuwa na sehemu saba…Utangulizi, Tanzania iliundwa mwaka 11964 kwa kuunganisha visiwa vya Bahari ya Hindi vya Zimbabwe na Pemba vilivyoungana na nchi ya Bara iliyokuwa ikiitwa Tanganyika…," alisema Naibu Waziri Mulugo kwa kujiamini na bila kuonyesha dalili yoyote kuwa alikuwa amekosea.
Naibu waziri huyo alikuwa akiwasilisha mada katika mkutano wa viongozi na wataalamu wa elimu katika Bara la Afrika, ambao ulifanyika Afrika Kusini kuanzia Oktoba 5-7, mwaka huu.
Kuboronga huko kwa naibu waziri huyo kumeibua mjadala mkubwa na mzito miongoni mwa Watanzania wa kada na rika mbalimbali, huku wengi wakianza kupata wasiwasi juu ya uwezo wa watu wanaoteuliwa na Rais Kikwete kushika nyadhifa mbalimbali serikalini.
Watu wengi waliotoa maoni yao juu ya suala hili kupitia mitandao ya kijamii ya Jamii Forum, Wanabidii, Facebook na Twiter wameonyesha wasiwasi mkubwa na kiwango cha elimu na weledi wa Mulugo na kuuliza swali; "elimu ya waziri huyu inatosheleza kumudu majukumu yake ya Naibu Waziri wa Elimu?"
Wasifu wa Naibu Waziri Mulugo uliopatikana kupitia mtandao wa Google, unaonyesha kuwa ana elimu ya shahada ya kwanza aliyoipata kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, kati ya mwaka 2002 na 2008.
Anadai katika wasifu huo kuwa kabla ya kuingia chuo kikuu, amesoma katika shule za sekondari za Songea Boys High School kwa masomo ya kidato cha tano na sita kuanzia mwaka 1994 mpaka 1996, na Sekondari ya Mbeya kwa masomo ya kidato cha kwanza mpaka cha nne kuanzia mwaka 1990 mpaka 1993.
Mulugo amejieleza kuwa kati ya mwaka 2000 na 2004 alifanya kazi ya ualimu katika Shule ya Sekondari Southern Highland, huku akiwa hajapata mafunzo yoyote ya taaluma ya ualimu.
Alipotafutwa kwa njia ya simu kufafanua alivyojieleza, Waziri Mulugo alisema alikuwa mjini Dodoma kuhudhuria kikao cha Baraza la Mawaziri, hivyo hakuwa na muda wa kuzungumza na gazeti hili.
 
 
 
Source; Tanzania Daima

Ray C Matatani?

According to The Kenyan Daily Post, controversial Tanzanian musician Ray C (full name Rehema Chalamila) has been admitted to rehab.
She showed an interest in singing at an early age, she spent her childhood between Dar Es Salaam and Uganda. Ray C first came to public attention as a radio DJ on Dar Es Salaam radio station Clouds FM. She took vocal and belly-dancing lessons and released her first album 'Mapenzi Yangu' in 2003. The album was a success in her native Tanzania, but it was the release of her sophomore attempt 'Na Wewe Milele' the following year that shot her to fame across East Africa.
On the back of the success of her second album, Ray C won Kilimanjaro and Kisima Music Awards as well as booking a raft of corporate performances. She released her third album, the self-titled Ray C in 2007.  At the height of her success a sex tape featuring the Taarab and Bongo Flava star was released, but the singer and dancer took it in stride.  Since the further nude images of Ray C have surfaced on the internet, but do not seem to have affected her popularity.
Ray C has performed globally, with appearances in The UK, The US, Germany, Sweden, China, Uganda, Nigeria, India, South Africa and Kenya.
The artist has recently returned a year spent in Kenya, where her music has been popular after she featured on a track called Moto Moto with Kenyan star French Boy. While in Kenya she continued to find herself mired in controversy, after making accusations against Kenyan promoter Sadat Muhindi and launching a tirade against Kenyan editor, Charles Otieno.

MSN

Monday, October 22, 2012

VIONGOZI WA UAMSHO WAFIKISHWA MAHAKAMANI


Viongozi wa Uamsho wafikishwa Mahakamani Zanzibar
Kufuatia vurugu za siku nne mfululizo huko Zanzibar, hii leo Sheikh Farid pamoja na viongozi wenzake wanne wa kundi la uamsho wamefikishwa mahakamani kujibu mashataka ya kusababisha vurugu.

Kiongozi wa Uamsho aibuka, anaswa Zanzibar

•  NI SHEIKH FARID ALIYEPOTEA NA KUSABABISHA VURUGU ZA KIDINI
na Ratifa Baranyikwa

BAADA ya kupotea kwa siku nne na kusababisha vurugu kubwa visiwani Zanzibar, Kiongozi wa taasisi ya Kiislamu ya Uamsho Zanzibar, Sheikh Farid Hadi Ahmed, ameonekana na kudai kuwa alitekwa nyara na polisi na maofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa.
Wakati Sheikh Farid akiibuka na kudai kuwa alitekwa, serikali kwa upande wake imemkamata na kumhoji ili kubaini kama kweli alitekwa au alijificha na kusababisha uvunjifu wa amani visiwani Zanzibar.
Sheikh Farid ambaye amekuwa mwiba mkali kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), alionekana majira ya saa 2:15 usiku wa kuamkia juzi katika eneo la Mazizini, nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Akizungumza na waandishi wa habari akiwa nyumbani kwake jana, Sheikh Farid aliibua madai mazito kwamba alitekwa nyara na polisi na maofisa wa Idara ya Usalama kwa lengo la kumhoji kuhusiana na harakati zake za kuitetea Zanzibar.
Jinsi alivyotekwa
Akisimulia jinsi alivyotekwa, Sheikh Farid alisema siku ya tukio alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kuwa ni mwanafunzi wake wa Madrasa ya Mahdi Mahfoudh na kumwomba wakutane katika eneo la Mbweni, karibu na duka ambapo mbele yake kuna msikiti mdogo usiosaliwa na watu wengi.
Alisema alitoka nyumbani kwake akiwa na kijana wake mmoja ambaye hakumtaja jina na wakati huo huo alikuwa anataka kununua umeme.
Alisema alipofika sehemu ya kununulia umeme, alimwomba kijana wake akamnunulie na yeye alingia  msalani kujisaidia.
“Kitendo cha yule kijana kuondoka tu na mie kutoka msalani, nikaliona gari moja nisilolifahamu, linakuja na kuegesha mbele ya msikiti na akashuka kijana mmoja, akaniita. ‘maalim’, kisha kunitaka niingie kwenye gari na kujitambulisha kuwa yeye ni askari polisi,” Sheikh Farid alisema.
Alisema wakati askari huyo akimtaka aingie kwenye gari, ndani ya gari hilo kulikuwa na askari wengine watatu waliokuwa na silaha za moto, hivyo hakuweza kufanya ubishi wa aina yoyote.
Kwa mujibu wa Sheikh Farid, baada ya kuingia kwenye gari, waliondoka kuelekea njia ya Uwanja wa Ndege, kisha kupita ‘round about’ kama mara nne ili kumpoteza lengo, asifahamu wapi anapelekwa na kuanzia hapo hakuweza kujua anaelekea wapi hadi alipofika katika nyumba hiyo.
“Nakumbuka walikuwa watu wanne walioniteka na kuniingiza kwenye gari. Nilipofika kwenye nyumba yao, muda wote nilikuwa nimefungwa kitambaa cheusi usoni, sikuruhusiwa kutembea sehemu yoyote ndani ya nyumba hiyo na kazi yangu ilikuwa kwenda chooni kujisaidia na kwa muda wa siku tatu niliokaa sijawahi kula chakula chohote zaidi ya kunywa maji,” alisema Sheikh Farid.
Sheikh huyo alisema wakati wa mahojiano alipata vitisho ili atoe maelezo yote kuhusiana na harakati zake na masuala mengi yalikuwa yakimlenga yeye binafsi, uhusiano wake na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein na uhusiano wake na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, pamoja na safari zake za kwenda na kurudi nchini Oman.
“Watu waliokuwa wananihoji walikuwa wakitofautina, kwani kila mmoja alikuwa akitumia namna yake. Baadhi walikuwa wakali na wengine walinihoji kwa utaratibu,” alisema Sheikh Farid.
Pia alisema walichambua simu yake kuangalia aina ya watu aliokuwa akiwasiliana nao na kwamba muda wote aliokuwa ndani ya nyumba hiyo hakuwahi kula chakula cha aina yoyote, kwani hakuwa na imani nao.
Alivyoachiwa na kurejeshwa uraiani
Sheikh Farid alisema juzi wakati anarudishwa, alishushwa ndani ya gari kama mzigo kwa kusukumwa huku akiwa ameendelea fungwa kitambaa usoni na umeme ukiwa umekatika.
Alisema sehemu aliyoshushwa ndiyo ile ile iliyotumiwa na vyombo hivyo vya dola kumteka na kuondoka naye.
Mara baada ya kushushwa katika eneo hilo, alisema alikwenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa mama yake eneo la Malindi ambapo alikutana na wafuasi wake wengi na kusalimiana nao, kisha akashauriwa kwenda Mbuyuni kwa mke wake mmoja ambaye anaishi eneo hilo karibu na Msikiti wa Mbuyuni.
Baada ya taarifa za kurejea kwa Sheikh Farid kuenea, mamia ya wafuasi wake walifika kwa wingi na kukaa nje ya geti la nyumba yake wakitaka kumuona kwani wengi hawakuamini kama angeachiwa akiwa hai.
Sheikh Farid aliwataka wafuasi wake watulie na wasifanye fujo huku akiwataka viongozi wa serikali kuwa waadilifu katika kushughulikia migogoro, akisema bila ya kutenda haki amani itatoweka.
“Licha ya kuniteka na kunitisha, sitarejea nyuma kamwe kuitetea Zanzibar hadi tone langu la mwisho, kwani ninachokifanya mimi na wenzangu ni kitendo kinachokubalika kisheria na hakuna wa kutuzuia,” alisema Sheikh Farid.
Alisisitiza kuwa wataitetea Zanzibar hadi iwe na dola na mamlaka kamili  na irudi katika hadhi yake kama ilivyokuwa mwaka  1963.
Waziri Nchimbi atoa kauli nzito
Katika hatua nyingine, serikali imesema kuwa inachunguza tukio la kutoweka na kurejea kwa Sheikh Farid na kusababisha vurugu na mauaji visiwani Zanzibar.
Tayari Jeshi la Polisi jana lilimhoji kwa saa kadhaa ili kubaini kama alijificha au alitekwa nyara kama anavyodai.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi, katika mkutano wake na waandishi wa habari.
Akizungumzia tukio hilo, Dk. Nchimbi alisema polisi walipata taarifa za kuonekana kwa Sheikh Farid jana asubuhi katika eneo la Mji Mkongwe.
Alisema Sheikh Farid alikuwa akihojiwa na polisi katika Kituo cha Mademwa jana ili kueleza mahali alikokuwa.
Wakati Dk. Nchimbi akieleza hayo, taarifa nyingine zinasema kuwa Sheikh Farid alijificha kwa makusudi ili kuleta vurugu.
Dk. Nchimbi alisema ikithibitika kwamba alijificha kwa makusudi ni kosa kisheria, kwa sababu kutoweka kwake kulisababisha uvunjifu wa amani.
Alisema kutoweka kwa Sheikh Farid Oktoba 16 mwaka huu Zanzibar kulisababisha vurugu na mauaji ya askari polisi, Koplo Said Abraham Juma, aliyeuawa kwa kukatwa mapanga Oktoba 18, mwaka huu.
Akizungumzia vurugu zilizotokea jijini Dar es Salaam siku ya Ijumaa zilizotokana na kukamatwa kwa Sheikh Ponda Issa Ponda, Dk. Nchimbi alisema kuanzia sasa serikali haitawavumilia wanaofadhili, wanaowatuma na wanaofanikisha vurugu hizo.
Alisema wanafanya uchunguzi kubaini kama kuna watu wanaowezesha maandamano ya Waislamu, kwa sababu wamegundua kuwa watu hao wamekuwa wanatumia magari na vipaza sauti kuzunguka mitaani ambavyo vinahitaji fedha.
Kuhusu tukio lililotokea Ijumaa alisema baada ya upelelezi serikali imebaini kuwa wafuasi wa Sheikh Ponda walijaribu kuwashawishi watu waende Ikulu ama sehemu nyingine kushinikiza kiongozi wao aachiliwe.
“Mahakama haijampa dhamana, hivyo kujaribu kushinikiza atolewe ni kosa kisheria na wanaingilia uhuru wa mahakama,” alisema Dk. Nchimbi.
Nchimbi alisema hakuna vurugu ama maandamano yatakayosaidia Ponda na wenzake watoke mahakamani.
Nchimbi pia ametangaza kusitisha mihadhara yote ya kidini nchi nzima kwa siku 30 mpaka hapo watakapoona namna bora ya kufanyika.
“Kuna watu ambao wanafikiri hawaguswi, wanasema wakiguswa moto utawaka, sisi tumekataa, kama moto ukiwaka uwake tutauzima…mkiandamana tunawakung’uta,” alisisitiza Dk. Nchimbi.
Aliongeza kuwa: “Tunakoelekea siko, tunaanza kutazamana kwa misingi ya kidini, kushabikia mpasuko wa kidini…sasa hivi kama kuna mtu amesikiliza hivi vyombo vya habari vya kimataifa…wanatoa taarifa kwa watalii wao wanaokuja huku kwamba Tanzania iko kwenye mpasuko wa kidini.
“Tunapelekwa sehemu ambayo watu wataacha kusalimiana, kupendana, tunajua athari za chokochoko za kidini, wenzetu Ulaya wanalifahamu hili vizuri ndiyo maana leo hii ni waangalifu sana, miaka 400 iliyopita watu milioni nne walikufa, Sudan watu karibu milioni mbili, Lebanon hadi waliposema sasa tukae tuzungumze, walikuwa wamepoteza maisha ya watu 250,000,” alisema.
Kwa mujibu wa Dk. Nchimbi, nchi yetu haitaki kufika huko na katika hilo alisisitiza serikali inakaribisha mazungumzo yasiyo ya vitisho na viongozi wa dini zote katika kujenga amani na utulivu wa nchi yetu.
Alisema serikali inawataka Watanzania kuheshimu dini za watu wengine na kwamba kudharau vitu vya ibada, kama kuharibu vitabu vya dini kama Kurani au Biblia, kushambulia waumini au majengo ya ibada ya dini nyingine ni kosa kisheria na havitavumiliwa.

Ikulu yajitetea kauli ya Ulimboka




Na Ratifa Baranyikwa
SIKU moja baada ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Nchini, Dk. Stephen Ulimboka, kusisitiza kwamba alitekwa na mtu anayefanya kazi Ikulu, Ramadhan Ighondu, Ikulu imehamanika na kujitetea kwamba madai hayo ni ya kipuuzi.
Juzi, Dk. Ulimboka alitoa tamko akisema kwamba Ighondu ndiye aliyehusika na sakata la kuteka na kumtesa vibaya, ambalo wengine wamekuwa wakiliita jaribio la kumuua; lakini jana katika hali inayoonyesha kwamba Ikulu haiko tayari kumchukulia hatua mtumishi wake anayetuhumiwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu, alisisitiza: “Ikulu iliishajibu. Tulisema haihusiki, na Rais Jakaya Kikwete amepata kuzungumza juu ya jambo hili mara nyingi.”
Wakati Ikulu ikimtetea mtuhumiwa huyo na kujaribu kujivua lawama, Jeshi la Polisi, ambalo lilimtia mbaroni raia wa Kenya na kumpeleka mahakamani kujibu tuhuma za kumteka na kumtesa daktari huyo, nalo limesita kubainisha kama litamkamata na kumhoji Ighondu, ambaye ametajwa rasmi na shahidi wa kwanza halisi katika suala hili, Dk. Ulimboka.
Badala yake maofisa wa jeshi hilo wametupiana mpira kila mmoja akidai hahusiki na suala hilo.
Katika tamko lake la kiapo lililotolewa kwa waandishi wa habari juzi, Dk. Ulimboka, kupitia kwa wakili wa kujitegemea, Nyaronyo Kicheere, alisema anamfahamu mtesaji wake, na kwamba hata akikamatwa leo hii, atakwenda kufanya utambuzi.
Alisema anashangaa kwamba polisi wameshindwa kumtia mbaroni mtuhumiwa huyo, licha ya kwamba alishatajwa na gazeti la MwanaHALISI na katika mtandao wa YouTube.
Alisema: “Nathibitisha kwamba Ramadhan Ighondu alitambulishwa kwetu kwa jina la Abeid. Binafsi ninamfahamu sana bwana huyu kwa sababu alikuwa akitumwa mara kwa mara kuja kukutana na mimi na tumekutana mara kadhaa kabla ya tukio lile.
“Nathibitisha kwamba mfanyakazi huyu wa Ikulu, ndiye aliyenipigia simu na kuniita kwenye kikao ambacho muda mfupi baadaye nilitekwa. Katika mawasiliano hayo, Abeid alikuwa anatumia simu namba 0713 760473.”
Dk. Ulimboka aliongeza kuwa anakumbuka kuwa Abeid alitambulishwa kwake na kigogo mmoja, akiwa na wawakilishi wengine wa madaktari, kuwa ndiye angehusika katika kuchukua madai na hoja za madaktari katika mgogoro kati ya madaktari na serikali.
Lakini Rweyemamu hakutaka kufafanua zaidi badala yake alisema, “Naomba uninukuu; haya madai ni upuuzi…hiki kitu kilishajibiwa.”
Alipoulizwa kama anamfahamu Ramadhan Ighondu, Rweyemamu alikwepa swali, huku akisisitiza kuwa Ikulu haihusiki naye.
Baada ya kuona swali hilo analikwepa, mwandishi alimuuliza Rweyemamu ni hatua gani ambazo Ikulu itamchukulia Ighondu kama mfanyakazi wao.
Swali hilo lilionekana kumkera Rweyemamu, akajibu kwa ukali, “Kama Ikulu haihusiki, hatuna cha kufanya juu ya jambo hilo; mnakaa mnalea maneno ya kipuuzi…Ikulu imwajibishe kuhusu nini? Haihusiki!”
Alipobanwa zaidi alisema kama kuna watu wanasema hivyo waende wakaripoti polisi.
Kauli ya jana ya Rweyemamu ni ya pili kutolewa na Ikulu kuhusu Dk. Ulimboka. Mara ya kwanza, ilipotolewa na Rais Jakaya Kikwete alipokutana na baadhi ya wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari, akasema, “Dk. Ulimboka ana nini mpaka Ikulu imteke? Tumteke ili iweje?”
Kikwete alikwenda mbali zaidi na kusema hata Dk. Ulimboka mwenyewe alipokwenda Ikulu akiwa na viongozi wenzake alinyamaza kimya tu na kwamba waliokuwa wakizungumza ni wengine.
Hata hivyo, kwa kuwa Ikulu imesema haihusiki, na Dk. Ulimboka mwenyewe ametamka kwamba anamjua aliyemtesa, na kwamba anafanya kazi Ikulu, ni juu ya umma kuamua nani anasema ukweli.

Tamko la Ulimboka kuhusu alivyotekwa na kijana wa Ikulu


Leo ikiwa ni takribani miezi mitatu imepita, huku nikiwa najiandaa kuelekea nje ya nchi kwa matibabu zaidi, nimekaa na kutafakari kwa makini na kugundua kuwa nitakuwa sijawatendea haki Watanzania ambao waliniombea kwa sala, dua na wengine kufunga, iwapo nitaondoka nchini bila kueleza au kuthibitisha japo kwa uchache, baadhi ya yale yalioandikwa na vyombo vya habari, hasa gazeti lililofungiwa na serikali kwa kuripoti tukio la kutekwa kwangu la MwanaHalisi.
Kabla ya kutoa andishi hili, nimejiuliza pia mambo mengi; kwa mfano, ni jukumu la nani kuhakikisha haki inatendeka katika nchi yetu? Ni jukumu la vyombo vya habari ambavyo hutajwa kuwa ni mhimili wa nne wa dola? Je, ni jukumu la Bunge? Je, ni jukumu la serikali ambayo imepewa nguvu za dola na wananchi?
Je, ni jukumu la asasi zisizo za kiserikali (Civil Society) ambazo wengine huita mhimili wa tano? Au ni jukumu la mhusika mwenyewe kuelezea kinagaubaga kilichompata na kwamba ni yeye pekee anayepaswa kupigania upatikanaji wa haki yake? Binafsi sikupata jibu.
Kutokana na kushindwa huko kupata majibu, ndipo kwa ustawi wa taifa langu nimeamua kueleza yafuatayo:
Kwamba tukio la kutekwa kwangu, kusukumizwa kwenye gari, kupigwa, kufungwa mikono na miguu, kunyofolewa kucha na kutolewa meno; na hatimaye kutupwa katika msitu wa Mabwepande, Wilaya Kinondoni, mkoani Dar es Salaam, lilitokea wakati nikiwa na kikao na afisa aliyetambulishwa kwetu kuwa ni afisa wa Ikulu, Ramadhani Abeid Ighondu.
Nathibitisha kwamba Ramadhani Ighondu alitambulishwa kwetu kwa jina la Abeid. Binafsi ninamfahamu sana bwana huyu kwa sababu alikuwa akitumwa mara kwa mara kuja kukutana na mimi na tumekutana mara kadhaa kabla ya tukio lile.
Nakumbuka kuwa Abeid alitambulishwa kwetu na kigogo mmoja, nikiwa pamoja na wawakilishi wengine wa madaktari kuwa yeye (Ramadhani Ighondu) ndiye atakayehusika katika kuchukua madai na hoja za madaktari katika mgogoro kati ya madaktari na serikali.
Nathibitisha kwamba mfanyakazi huyu wa Ikulu, ndiye aliyenipigia simu na kuniita kwenye kikao ambako muda mfupi baadaye nilitekwa. Katika mawasiliano hayo, Abeid alikuwa anatumia simu Na. 0713 760473.
Kwamba hakuna mashaka kwamba namtambua Abeid kwa sura na namba aliyokuwa anatumia kuwasiliana nami mpaka siku ya kutekwa kwangu. Ni namba hiyo hiyo iliyoandikwa na gazeti tajwa hapo juu.
Katika mawasiliano hayo, mimi nilikuwa natumia simu 0713 731610 na kwamba mimi naamini kwa dhati kuwa afisa huyo wa Ikulu bado yuko hai na mimi na wenzangu tuko tayari kutoa ushirikiano kwa chombo huru kuhakikisha haki inatendeka.
Aidha, kwa nyakati tofauti Abeid alitumwa kwangu kukagua/kuchukua nyaraka zangu mbalimbali ikiwa pamoja na vyeti kwa ajili ya uthibitisho wa taaluma na masomo yangu.
Siku ya kwanza ya utambulisho akiwa pamoja na afisa mwenzake wa Ikulu, Ramadhani alichukua maelezo mafupi ya mtiririko wa mgogoro na akaendelea kufanya hivyo kwa nyakati tofauti.
Ninaendelea kuthibitisha kuwa maelezo niliyotoa ambayo yamerekodiwa kwenye mitandao mbalimbali pamoja na kwenye mtandao wa intaneti wa YouTube kuwa ni maelezo ya kweli.
Wakati natoa maelezo hayo nilikuwa nipo na kumbukumbu nzuri bila athari yoyote pamoja na maumivu makali ya mwili na kupungukiwa damu.
Uthibitisho wa kumbukumbu nzuri niliyokuwa nayo, ni pale nilipokutana na Juma Mganza katika msitu wa Mabwepande asubuhi ya siku ya tukio. Pamoja na maumivu makali niliyokuwa nayo kutoka kila sehemu ya mwili wangu, niliweza kumshawishi Mganza kunifungua kamba za mikono nilizokuwa nimefungwa.
Na pia kukumbuka namba ya simu ya rafiki yangu Dk. Deogratias ambapo Mganza aliweza kuitumia kuwasiliana naye kumpa taarifa juu ya tukio hilo. Ni kupitia taarifa hiyo, ndipo suala la mimi kufikishwa hospitali ya mifupa MOI lilipofanikiwa.
Najua wapo watu ambao wamekuwa wakihaha kupindisha ukweli. Lakini wanaotaka kupindisha ukweli wanasahau kuwa, kama niliweza kushawishi Juma Mganza hadi akashawishika kunikaribia na kunisikiliza pamoja na hofu aliyokuwa nayo ya kukutana na mtu aliyekuwa kwenye hali kama yangu.
Na kama niliweza pia kukumbuka namba ya rafiki yangu, mambo hayo yanatosha kuthibitisha kuwa nilichokisema ni ukweli na kuwa utimamu na kumbukumbu zangu ni sahihi.
Hivyo basi, nathibitisha kuwa maelezo yote niliyotoa na kurekodiwa kabla sijafika na kwamba Watanzania wawapuuze wale wote wanaotaka kupotosha ukweli juu ya jambo hili.
Ninaendelea kuthibitisha kuwa Abeid ninamfahamu na hata akikamatwa leo hii, nitakwenda kufanya utambuzi. Inasikitisha kukumbusha kuwa hatujasikia popote kuwa Abeid pamoja na washiriki wake wamehojiwa pamoja na jamaa wengine waliotajwa mpaka sasa.
Ninafahamu kuwa ibara ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa kinga kwa uhai wa kila mtu anayeishi katika nchi yetu. Tena inaitaka jamii kulinda uhai wa kila mtu.
Mimi Ulimboka Stephen ni raia wa Tanzania ambaye ninafahamu kuwa nina haki ya kuishi na kuwa serikali yangu na wananchi wenzangu wana jukumu la kuulinda uhai wangu.
Kilicho na kinachonisikitisha sana ni kuona jinsi serikali ya nchi yangu ilivyopuuza kuhatarishwa kwa uhai wangu na kutoa kauli za rejareja juu ya unyama huo. Wale wote waliotuhumiwa na ninaowatuhumu kunitendea unyama huu wako huru na hakuna aliyewagusa.
Je, uhai na maisha yangu yana thamani ndogo kama ya mnyama anayekwenda machinjioni? Je, serikali ya nchi yangu itakubali lini kuundwa kwa tume huru kuchunguza unyama huu na kuhakikisha kuwa haki inatendeka?
Je, kuna watu ambao katika nchi yetu ambao wana haki ya kutenda unyama kwa kuwa wao wako juu ya sheria? Hiyo siyo Tanzania ninayoifahamu au ambayo Watanzania wenzangu wanaipenda na kuwa tayari kuifia.
Ninapenda kusema kuwa mimi niko tayari kuhojiwa na kutoa ushirikiano wangu kwa vyombo huru na makini vya uchunguzi ambavyo vitaundwa ili kuweza kuubaini ukweli.
Kwa madaktari wenzangu ninapenda kusema kuwa niko pamoja nao na kuwa madai yetu ni ya haki na ya msingi. Nitaendelea kuwa nao katika kupigania masilahi yetu na kuwa tusikubali kugawanywa na watu wasiotutakia mema na wanaoishi kwa vitisho na si hoja.
Sisi kama madaktari tunastahili kufanya kazi katika mazingira mazuri na kupata ujira wa haki kutokana na kazi na huduma yetu tukufu.
Namaliza kwa kusema wapo watu ambao hawatapenda kusikia siri iliyojificha katika tukio lile. Lakini nimetafakari sana, nimeona hakuna njia nyingine iliyonyooka zaidi ya kueleza ukweli na kama ilivyoandikwa katika vitabu vitakatifu “ukweli utawaweka huru”.

Friday, December 5, 2008

MISA- Media Institute of Southern Africa

ZIMBABWE, Harare : Zimbabwe central bank governor Gideon Gono speaks at a press conference to discuss the dismissal of the entire board of a local bank, CFX Holdings after it was leaked that the bank had off-loaded 260 billion Zimbabwe dollars of the new currency to buy foreign exchange one day before the notes were legal tender on December 4, 2008 in Harare. Once described as a model economy and a regional breadbasket, Zimbabwe's economy has collapsed over the past decade and there are now shortages of basic foodstuffs like sugar and cooking oil.

Friday, November 14, 2008

Woow! Thanks God


This was the first internet related workshop for me, my be it won't be the last.
The training was organized by MISA in collaboration with the VIKES Foundation of Finland; the International Solidarity Foundation of the Union Journalists and other Finnish media organizations.
We were 19 participants coming from media houses, colleges, and universities. In fact it was the great place were we had chance to know each other and share diverse experiences.!In fact the class was so wonderful, Thanks God.
Our facilitator, Mr Peik Johansson from Finnish Broadcasting Company YLE Radio Finland , showed and tought us on how people in Finland and other European countries get their services done via internet. We checked on how to purchase ticket via Internet and we went further by visiting some local and international websites.
In day two, Mr. Peik showed us how to make a blog, and we started blogging and making new posting to our blogs that we created.
The following day, we had the assignment of posting ideas we got after yesterday training by using our source which was a speech by Rupert Murdoch.
After class we had a reception party at the embassy of Finland it was so fun!
Also we had a time to visit local and international websites and made comments for what we h’ve seen good and bad, the same day we learned how we could link our blog with local and international websites.
Then the last day we had a guest lecturer at our workshop, Maggid Mjengwa, I knew him
The guy presented to us his blog http://www.mjengwa.blogspot.com/
Mr Maggid showed us how to add picture (s) in our blogs. The lesson added value to our blogs, now you can see pictures in there.
Comments
In short we learnt a lot of things related to internet surfing and blogging. Since then, I found myself becoming a constant visitor of websites, using it as on of the tools of information.

In fact, I came to realise that, perhaps I needed more time than a week to become a mogul in the field.
Thanks MISA, thanks Finland for doing such a wonderful thing to us.
Ooh thanks Peik, you are such a wonderful teacher, I learnt so many things from u' I'll remember you always.

Our teacher, Mr Peik

Jamani hapa ndio tupo darasani, darasa limekolea kweli kweli, aliyesimama Mr Peik, mwenye nguo ya Orange ni Nancy Mwendamseke, yeye ni Head wa Department ya Mass Communication, Tumaini University hapa Dar es Salaam, mwenye nguo ya Kijani ni mimi mwenyewe Ratifa Baranyikwa.

We are in the Classroom


In the classroom with my fellow students. From left Nancy Mwendamseke, myself (Ratifa Baranyikwa) followed by Jacqueline Maro then Abbas El-Sabri, Edwin Mpokasye and Lillian Timbuka. (Photo by Maggid Mjengwa)

Thursday, November 13, 2008

Day 4, Assignment

7 World Trade Center
World Trade Center is a building based in New York City, America located across from the World Trade Center site in Lower Manhattan. The name "7 World Trade Center" has referred to two buildings: the original structure, completed in 1987, and the current structure.

The original one was destroyed on September 11, 2001, The attack shocked the world.
but now the original one replaced with the new 7 World Trade Center, which opened in 2006. Both buildings were developed by Larry Silverstein, who holds a ground lease for the site from the Port Authority of New York and New Jersey.
The original 7 World Trade Center was 47 stories tall, clad in red exterior masonry, and occupied a trapezoidal footprint. An elevated walkway connected the building to the World Trade Center plaza.

The building was situated above a Consolidated Edison (Con Ed) power substation, which imposed unique structural design constraints. When the building opened in 1987, Silverstein had difficulties attracting tenants. In 1988, Salomon Brothers signed a long-term lease, and became the main tenants of the building. On September 11, 2001, 7 WTC was damaged by debris when the nearby North Tower of the WTC collapsed.

The debris also ignited fires, which continued to burn throughout the afternoon on lower floors of the building, with a lack of water to fight the fires. The building collapsed completely at 5:20 p.m., when a critical column on the 13th floor buckled and triggered structural failure throughout.

The new 7 World Trade Center construction began in 2002 and was completed in 2006. It is 52 stories tall and still situated above the Con Ed power substation. Built on a smaller footprint than the original to allow Greenwich Street to be restored from TriBeCa through the World Trade Center site and south to Battery Park, the new building is bounded by Greenwich, Vesey, Washington, and Barclay streets.

A small park across Greenwich Street occupies space that was part of the original building's footprint. The current 7 World Trade Center's design placed emphasis on safety, with a reinforced concrete core, wider stairways, and thicker fireproofing of steel columns, and incorporates numerous environmentally friendly features.

ENDs

Tuesday, November 11, 2008

Workshop

It was Monday, 10th November 11, 2008 My self was happy as I arrived at Tanzania Global Development Learning Centre (TGDLC), Dar es Salaam

I met Peik Johansson, Our trainer, from Finnish Broadcasting Company YLE Radio Finland.
Dear friends the man tought us how Internet has changed societies and communication globaly
Actually,I learned a lot of things which I didn't know before.